Isaiah 60:12-14

12 aKwa maana taifa au ufalme ule ambao hautakutumikia utaangamia;
utaharibiwa kabisa.

13 b“Utukufu wa Lebanoni utakujilia,
msunobari, mvinje pamoja na mteashuri,
ili kupapamba mahali pangu patakatifu,
nami nitapatukuza mahali pa miguu yangu.
14 cWana wa wale waliokuonea watakuja wakisujudu mbele yako,
wote wanaokudharau watasujudu kwenye miguu yako,
nao watakuita Mji wa Bwana,
Sayuni ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Copyright information for SwhNEN